Kwa watu wanaojiajiri, unaweza kulipa kupitia pesa kwenye simu, kuwasilisha kutoka kwa benki hadi bendi, au vituo vya malipo vilivyoidhinishwa.
Malipo ya mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA) ni sehemu ya juhudi za serikali kuhakikisha upatikanaji wa Huduma ya Afya kwa Wote (UHC) kwa Wakenya wote. Malipo ya SHA na taratibu za malipo hutegemea kama wewe ni mwajiriwa au unajiajiri.
Ili kutoa malipo yako ya SHA, unaweza kutumia njia zifuatazo:
1. Malipo kupitia mwajiri: Hii inawahusu watu walioajiriwa rasmi. Mwajiri wako atakata malipo yako ya SHA moja kwa moja kutoka kwenye mshahara wako na kuuwasilisha kwa SHA. Hii ni sawa na makato mengine ya kisheria kama malipo ya uzeeni ya NSSF.
2. Malipo kwa watu wanaojiajiri: Unaweza kujisajili na kulipa kwa hiari. Malipo yanaweza kufanywa kwa kutumia M-Pesa au majukwaa mengine ya pesa za simu, hamisho la pesa kwa benki, au vituo vya malipo vilivyoidhinishwa.
Huenda ukahitaji kuingia kwenye tovuti ya SHA au kutembelea kituo cha huduma kama Huduma Centre, vituo vya SHA, au vituo vilivyowekwa hospitali kwa ajili ya kujisajili na kupata maelezo ya malipo yako.
Kwa watu wanaojiajiri, SHA hutumia mfumo wa kupima uwezo wa kipato (Means Testing) ili kuhesabu bima ya afya kwa familia zisizo na kipato cha kudumu kila mwezi.
Jinsi ya kupata huduma ya kupima uwezo wa kipato (Means Testing)
Nenda kwenye afyayangu.go.ke
Bofya Maelezo Yangu (My Profile).
Bofya Mapato (Income) na uonyeshe kuwa umejiajiri.
Jibu maswali yaliyo chini ya kupima uwezo wa mapato (Means Testing).
SHA itahesabu kiasi unachohitajika kulipa kila mwezi au kila mwaka kulingana na majibu yako.
Mpango wa kupima uwezo wa mapato huzingatia mambo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kama:
- Wanafamilia
- Hali ya makazi
- Uwezo wako wa kupata huduma za msingi
- Umiliki wa mali
- Elimu
- Ajira
Kulingana na majibu yako, kiwango cha malipo yako kitahesabiwa na utaonyeshwa kiasi cha kulipa kwa kila mwezi au kila mwaka.
Baada ya kupata kiasi hicho utakacho hitajika kulipa, unaweza kutumia njia mbalimbali za kulipa bima yako.
Hatua za kulipa kupitia Paybill ya M-Pesa
- Fungua menyu ya M-Pesa kwenye simu yako.
- Chagua “Lipa na M-Pesa.”
- Chagua “Paybill.”
- Weka nambari ya Paybill: 200222.
- Kwa nambari ya akaunti, weka nambari yako ya Kitambulisho cha Taifa (ID).
- Weka kiasi cha pesa unachotakiwa kulipa.
- Kamilisha kwa kuingiza PIN ya M-Pesa.
Malipo kwa kutumia njia ya USSD
- Piga *147#.
- Weka nambari yako ya Kitambulisho cha Taifa (ID) utakapoitishwa.
- Chagua chaguo la Lipa (Make Payment).
- Fuata maelekezo yanayofuata ili kukamilisha malipo.
Malipo kupitia tovuti
- Nenda kwenye tovuti ya Afya Yangu.
- Ingia kwenye akaunti yako kwa kuandika nambari yako ya kitambulisho cha taifa na kuunda nenosiri la wakati moja OTP.
- Nenda kwenye sehemu ya malipo (payment section).
- Fuata maelekezo yaliyotolewa ili kufanya malipo.
Vidokezo Muhimu:
Hakikisha umeingiza nambari yako ya ID kwa usahihi kama nambari ya akaunti ili kuepuka matatizo ya malipo.
Baada ya kufanya malipo, ni vyema kuthibitisha kuwa malipo yamefanikishwa kwa kukagua akaunti yako ya SHA au kuwasiliana na huduma kwa wateja wa SHA.
Ukipata changamoto wakati wa malipo, wasiliana na huduma kwa wateja wa SHA au tembelea kituo cha huduma kilicho karibu nawe ili kupata usaidizi.
Unaweza kutembelea tovuti rasmi ya SHA kwa taarifa zaidi na usaidizi.



